Thursday, 13 April 2017

MAJINA YA WALIMU WA SAYANSI WALIOPATA AJIRA



SeeBait
Serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI imetangaza ajira mpya kwa Walimu wa masomo ya Hisabati na Sayansi leo tarehe 12 Aprili, 2017.

Majina ya Walimu yaliyotangazwa yanatokana na tangazo la nafasi ya kazi ya Ualimu lililotolewa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia mnamo tarehe 01 Desemba, 2016.
 
Jumla ya Walimu wapya wapatao 3,081 wakiwemo 1,544 ni wa ngazi ya Shahada na Walimu 1,537 ni wa Stashahada.
 
Walimu hao watatakiwa kuripoti kwenye Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri na baadaye kwenye Shule walizopangiwa kuanzia tarehe 18 Aprili, 2017 hadi tarehe 25 Aprili, 2017. Walimu wote waripoti wakiwa na vyeti halisi vya taaluma vya kidato cha nne (IV) na kidato cha sita (VI), vyeti halisi vya kitaalaam vya kuhitimu mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada na Shahada na Cheti cha kuzaliwa.
 
Angalizo :
i. Walimu waliopangiwa vituo ni wa masomo ya Hisabati na Sayansi waliohitimu hadi mwaka 2014/2015.

ii. Kituo cha kazi cha mwalimu ni shule aliyopangiwa na sio makao makuu ya Halmashauri.
 
iii. Mwalimu atakayeripoti na kuchukua posho ya kujikimu na baadae kuondoka atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria.
 
iv. Walimu wote watakiwa kuripoti katika vituo vyao kuanzia tarehe 18 Aprili, 2017 hadi 25 Aprili, 2017, watakaochelewa nafasi zao zitajazwa na mwalimu mwingine.
 
v. Hakutakuwa na uhamisho ndani ya Mkoa au Halmashauri.
Majina ya Walimu hao yanapatikana katika tovuti ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI ya www.tamisemi.go.tz
 
Imetolewa na:
Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais TAMISEMI

==>Orodha ya Walimu wa Shahada wa Ajira Mpya kwa Masomo ya Sayansi na Hisabati.



==>Orodha ya Walimu wa Ajira Mpya kwa Masomo ya Sayansi na Hisabati.

Wednesday, 5 April 2017

MBIO ZA UBINGWA ZA ZIDI KUNOGA ENGLAND


Bildergebnis für hazard

Magoli ya Eden Hazard ya dakika ya 10 na 35 yazidi kuiweka chelsea kileleni ikishinda nyumbani zidi ya mancherster city 2-1, huku Aguero akifunga bao pekee la mancherster city dakika ya 26. ushindi huu unaiweka chelsea kileleni point 7 juu ya tottenham walioko nafasi ya pili kwenye ligi hiyo.mechi nyingine,HULL CITY 4 - 2 MIDDLESBROUGH,SWANSEA CITY 1 - 3 TOTTENHAM
HOTSPUR,SOUTHAMPTON 3 - 1 CRYSTAL PALACE,LIVERPOOL 2 - 2 AFC BOURNEMOUTH.ARSENAL 3 - 0 WEST HAM UNITED.ligi itaendelea wikendi hii.

MATOKEO YA UCHAGUZI WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI(EALA)

Jana Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipiga kura kuchagua wabunge watakaoiwakilisha nchi katika Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EALA) kwa kipindi cha miaka mitano.

Baada ya mvutano wa muda mrefu kuhusu uchaguzi huo, ulifanyika na Spika wa Bunge, Job Ndugai kutangaza orodha ya washindi waliochaguliwa kuiwakilisha nchi.

Tanzania inatakiwa kutoa wabunge 9 kwenda EALA, lakini matokeo ya jana yalitangaza washindi saba tu baada ya wagombea wawili kupigiwa kura nyingi za hapana, na hivyo kuonekana kuwa wabunge hawakuwataka.

Kati ya wabunge 7 waliotangazwa, 6 ni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na mmoja na wa Chama cha Wananchi (CUF).

Wagombea wa CHADEMA, Lawrence Masha na Ezekiah Wenje walipingwa kwa kupigiwa kura nyingi za hapana.
  1.      Fancy Nkuhi (CCM)
  2.     Happiness Legiko (CCM)
  3.     Maryam Ussi Yahya (CCM)
  4.     Dkt Abdullah Makame (CCM)
  5.     Dkt Ngwaru Maghembe (CCM)
  6.     Alhaj Adam Kimbisa (CCM)
  7.     Habib Mnyaa (CUF)
Baada ya matokeo hayo kutangazwa, Mwenyekiti wa CHADEMA na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge alisema kuwa, hawayakubali matokeo hayo na kuwa watakwenda mahakamani.

Mbowe pia amemtuhumu Rais Dkt Magufuli na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuhusika katika mchakato wa kuwakataa wagombea wa CHADEMA na kusema kuwa, wao hawatakubaliana na hilo kwa sababu Spika wa Bunge amekiuka kanuni za bunge, na uchaguzi wote ulikuwa na kasoro